ads

Monday 9 January 2017

UNAPOJARIBIWA - BAHATI BUKUKU











[Unapojaribwa, usitende dhambi,
unapojaribiwa, jua Mungu yupo,
unapojaribiwa, usivunjike moyo,
hilo jaribu lako Mungu ameliona.] x2

jaribu ni mlango, wa kuinuliwa,
jaribu ni daraja la mafanikio,
jarbu ni darasa la watakatifu,
nimejifunza hilo kwa kuwa Mungu amefanya,
wakati wa jaribu watu wanakucheka,
wakati wa jarabu unadharauliwa,
wakati wa jaribu unajiona mpweke,
hilo jaribu lako Mungu ameliona.

unapojaribiwa, usilipe kisasi,
unapojaribiwa usimchukie huyo,
unapojaribiwa usitazame adui yako,
wewe mtazame Mungu umwombe rehema,
wakati wa jaribu, ikiwezekana,
huyo anayetumiwa muombee rehema,
wakati wa jaribu, Mungu akikupa neema,
pema na matatizo lia pamoja naye,

inawezekana, uko kwenye mateso,
inawezekana, umekata tamaa,
inawezekana, umedharauliwa,
hilo jaribu lako, Mungu ameliona,
inawezekana, ni wakati wa mateso,
inawezekana, marafiki wamekimbia,
inawezekana, ndugu amekutenga,
hilo jaribu lako Mungu atalijibu,
inawezekana uko wakati mbaya,
inawezekana kipindi cha kuonewa,
inawezekana, marafiki wamekutenga,
hilo jaribu lako, Mungu ameliona,
muombe Mungu, jibu lako liko,
muombe Mungu, leo atatenda,
muombe Mungu leo atakujibu,
hilo tatizo lako Mungu analijua,

[usikate tamaa, mwamini Yesu
usikate tamaa, mwambie Yesu] x10





www.gospelyrix.com







No comments:

Post a Comment