ads

Monday 9 January 2017

DUNIA HAINA HURUMA - BAHATI BUKUKU











Dunia-a-a-a-a.
dunia haina huruma x2
dunia haina faida,
dunia haina undugu,
na maisha yangu,
dunia haina huruma mwenzetu nasema,
asubuhi na mapema simu ya mkononi inaita,
naitazama kwa makini ni number ya mume wangu,
sauti ya kike inasikika, inayorarua moyo wangu,
moyo wangu unafura hasira, kwa taarifa ninazo pata,
haloo, neenda muhubir kachukue mzoga wako,
nikamuuliza ni nani mwenzangu, ananijibu kwa kejeli,
mimi ni mke mwenzio kama hutaki kunichezea,
nawatafuta ndugu na jamaa waliokuwa kwa simu yangu,
ili niwaambie taarifa hizi zilizo rarua moyo wangu,
dunia, haina huruma,
ninafika hosipitali,
nawapata watu wa mochari maneno wanayoniambia yananiumiza moyo wangu,
aaah yule mgonjwa aliyeletwa jana aliyepigwa kwenye ufumanizi,
tulipomwangalia tuligundua hajafa kwa hivyo yumo kwenye chumba cha watu maututi,
ninafika kwa chumba cha wagonjwa matuti,
ninakuta mpenzi wa roho yangu amepoteza fahamu hawezi nitazama,

[hili ndilo patano letu mume wangu,
hapa ndipo jijini mbea, mume wangu,[ x2

haya mapanga ndiyo zawadi yangu mume wangu,
hili ndilo patano letu mume wangu,
na hapa ndipo jijini mbea mume wangu,
nimegundu dunia hii, huruma eeh
dunia haina huruma, x2
dunia haina fadhira eeh,
wanadamu nisaidie,
nani mwenye huruma anifariji oh,
(maana moyo wangu unavuja damu) x2
kwa matatizo niliyopata,
dunia haina huruma,
dunia haina uchungu,
ninawapigia ndugu wa mume wangu,
waliomsibu mume wangu,
wote wananisusia,
nachukua vitabu vya benki,
ATM hazisomi zote,
namwomba daktari, daktari naomba nisaidie,
mume wangu akipona, gharama zote tutalipa,
na kama la gari langu utalichukua,
kwa kweli mama ngekusaidia,
lakini gari za aina hiyo zinavuja mafuta,
nawatafuta marafiki wa mume wangu,
ninapofika hapo, wananipa masharti yanararua moyo wangu,
nikimtazama mume wangu,vile kwanza anavyokoroma,
nikimtazama daktari hawezi ata kunitazama,
dunia haina huruma, x2
mashemeji wamegoma kutoa misaada, maneno wanayoniambia,
nawatafuta mawifi kwa mara nyengine,
niliamua kumwangukia daktari,
hicho ndicho chanzo cha tatizo langu,
ndiyo siku niliyo pata huyu mtoto,
msiba wangu ukaongezeka,
dunia haina huruma
dunia haina uchungu,
mimi na maisha yangu,
leo nataka kutengeneza na wewe,
nimechoka kudanganya moyo wangu,
nataka kutengeneza na wewe,
nimechoka kudanganya moyo wangu,
nataka kutengeneza na wewe,
lazima nitengeneze na wewe,
nikimwambia mume wangu, anaweza kuniua,
ila moyo wangu unanishuhudia, lazima nimwambie,
lakini nataka kutengeneza na wewe,
mimi lazima nitengeneze na wewe,
nimeamua nitengeneze na wewe,
nataka kutengeneza na wewe,

mume wangu alinitazama tu akaondoka mbele yangu,
asubuhi na mapema nikaitwa kijijini,
wakinisisitiza kwa hasira, kuja na mtoto wako akiwa hai,
nilipofika kijijini, nikawakuta mawifi zangu,
kila niliyesalimia hakuweza itikia,
mashemeji walionipenda, nao pia nilifanya hivyo hivyo,
ila aliye nitazama alinitazama kwa dharau,
huruma yangu iko wapi dunia, x2
kikao cha familia kilipokaa,
kiliomba wangu ndiye aliyenihukumu
nikamtazama mtoto wangu
aliyesimamishwa mbele yangu,
nikageuka pembeni yangu nikamwona mzee wangu,
alinitazama kwa hasira, asiweze nihurumia,
huruma yangu iko wapi dunia,
faraja yangu iko wapi dunia,
kimbilio yangu nikimbilie wapi dunia,
dunia ooh haina nuruma,
dunia haina fadhira,
ulimwengu nisaidie,
ulimwengu nihurumie,
nilipoendelea kuomba msamaha ,
wifi mkubwa aliinitishia,
bwana mmoja mwenye busara,
akasimama na kusema nani mmoja wetu hajawai tenda dhambi,
awe wa kwanza kupiga panga,
wote wakatazamana,
hakuna aliye niangalia,
mume wangu akasimama na kuanza kulia kwa uchungu,
kwanzia leo hii nisamehe mke wangu,
ya ulimwengu yamenichosha,
kwanzia leo hii ninatubu mke wangu,
nataka kutengeneza na Mungu,
kumbe Mungu anaweza kusamehe,
kumbe Mungu anaweza jibu maombi,




www.gospelyrix.com







1 comment:

  1. The lyrics provided don't match with the song. Please rectify.

    ReplyDelete